chirwa akabidhiwa mchezaji Amissi Tambwe ambaye sasa ni majeruhi alisema kocha mkuu wa yanga George Lwandamila

Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamina, amemkabidhi Obrey Chirwa majukumu ya Amissi Tambwe ambaye kwa sasa ni majeruhi.
Chirwa amepewa majukumu hayo kutokana na Tambwe kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu akiuguza majeraha ya goti.
Kutokana na kuuguza majeraha hayo, ilisababisha Tambwe akose mechi tano za kimashindano ambazo tayari Yanga imecheza ikiwa moja ya Ngao ya Jamii na nne Ligi Kuu Bara.
“Kukosekana kwa Tambwe hakuna tatizo lolote lile kwani Chirwa yupo, ninachokifanya ni kwamba kwenye kikosi changu natengeneza ile hali kwamba akikosekana mmoja basi anakuwepo mwingine wa kuziba pengo lake,” alisema Lwandamina.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger