Mazishi ya mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Mwimbaji huyo aliyetesa kwa sauti yake tamu na kwa tungo zake za kusisimua, amezikwa katika makaburi ya Kisutu huku idadi kubwa ya wanamuziki wa fani mbalimbali ikiwa sehemu ya umati uliofurika makaburini hapo. Aidha, Dede pia amezikwa na vigogo wengi wa dini ya Kiislam, maofisa wengi wa serekali na wanamichezo maarufu. Pengine kwa miaka ya hivi karibuni, ukiondoka msiba wa marehemu Muhudini Gurumo, hakuna tena msiba wa mwanamuziki wa dansi uliohudhuriwa na watu wengi kama huu wa Dede. Mwili wa Dede ukiswaliwa swala ya mwisho katika msikiti wa Makonde, Kariakoo Safari ya kuelekea makauburini inaanza Umati wa watu ukiondoka Kariakoo kuelekea makaburi ya Kisutu Kila mtu alitamani kubeba...
ALIYEKUWA kocha wa Panone FC, Jumanne Ntambi amejiunga na Mwadui FC kuchukua nafasi ya Ali Bushir aliyetupiwa virago. Ntambi aliyewahi kuifundisha Mwadui miaka ya nyuma, amesaini mkataba wa kukinoa kikosi hicho kwa msimu ujao. Katibu mkuu wa Mwadui, Ramadhani Kilao alisema Kocha huyo ataungana na Khalid Adam aliyekuwa kocha msaidizi wa Julio na Bushir. Alisema kuwa kati ya makocha hao, baada ya kusaini mkataba wanaangalia nani atakuwa kocha mkuu kwa sababu wote wanalingana kiwango cha elimu ambacho ni leseni ‘B’. “Baada ya kumuondoa Bushir tumemleta kocha mwingine anaitwa Ntambi, anaendelea na mazoezi na timu lakini kesho (juzi), ndio atasaini mkataba ila tutaangalia nani atakuwa kocha mkuu yeye na Khalid,” alisema Kilao.
Arsene Wenger amemuorodhesha winga wa Manchester United Anthony Martial katika orodha yake ya washambuliaji anaotaka kuwanunua kiangazi hiki. Kocha huyo wa Arsenal ameanza kumkatia tamaa kinda wa Monaco Kylian Mbappe na sasa anampigia hesabu Martial. Wenger anajiandaa kulipa pauni milioni 40 kwa Martial, ambaye amekosa nafasi ya kudumu Old Trafford chini ya Jose Mourinho. Hata hivyo Wenger anahofia kuwa Mourinho anaweza kumbania kutokana na uhasimu mkubwa ulioko kati yake na kocha huyo wa Manchester United.
Comments
Post a Comment