Mazishi ya mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Mwimbaji huyo aliyetesa kwa sauti yake tamu na kwa tungo zake za kusisimua, amezikwa katika makaburi ya Kisutu huku idadi kubwa ya wanamuziki wa fani mbalimbali ikiwa sehemu ya umati uliofurika makaburini hapo. Aidha, Dede pia amezikwa na vigogo wengi wa dini ya Kiislam, maofisa wengi wa serekali na wanamichezo maarufu. Pengine kwa miaka ya hivi karibuni, ukiondoka msiba wa marehemu Muhudini Gurumo, hakuna tena msiba wa mwanamuziki wa dansi uliohudhuriwa na watu wengi kama huu wa Dede. Mwili wa Dede ukiswaliwa swala ya mwisho katika msikiti wa Makonde, Kariakoo Safari ya kuelekea makauburini inaanza Umati wa watu ukiondoka Kariakoo kuelekea makaburi ya Kisutu Kila mtu alitamani kubeba...
KIUNGO mshambuliaji wa Azam FC, Ramadhan Singano (Messi) amemuwahi mwenzake Simon Msuva baada ya kuondoka nchini juzi kujiunga na klabu ya Difaa Hassan D’Eljadida iliyoshiriki ligi kuu nchini Morocco. Messi ambaye mkataba wake umemalizika hivi karibuni na klabu yake ya Azam amekwenda nchini Morocco kwa ajili ya kujiunga na klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo yenye timu 16. Wakati Messi akiondoka nchini humo winga wa Yanga, Simon Msuva ambaye naye anapigiwa hesabu na klabu hiyo anatarajia kuondoka nchini alhamisi hii ili kujiunga na klabu hiyo. Meneja wa Azam, Philp Alando alipoulizwa kuhusu safari ya winga huyo alisema kuwa klabu hiyo aina taarifa na lolote lile kwa kuwa walimalizana naye toka mkataba wake umemalizika. “Mkataba wa Singano ulikuwa umemalizika Julai 8 mwaka huu hivyo sisi hatuna mazungumzo naye yoyote na wala hatujui kuhusu safari hiyo ya Morocco wala chochote kinachoendelea,” alisema. Wakati ...
MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini. Kila timu imeshaangusha pointi Ni timu tano tu ambazo hazijapoteza mchezo katika ligi kuu msimu huu. Mtibwa, Azam FC, Simba, mabingwa watetezi Yanga na Tanzania Prisons, lakini zote hizo tayari zimeangusha pointi msimu huu huku Mtibwa na Azam FC wakiwa pekee waliangusha alama chache (mbili) baada ya kila timu kucheza michezo minne. Simba tayari wameangusha pointi nne, sawa na Yanga na Prisons ambazo zimeshinda michezo miwili na kupata sare katika michezo mingine miwili. Hii inamaanisha ligi imeanza kwa ugumu licha ya washambuliaji kuonekana kuwa na ‘usongo’ wa kufumania nyavu. Wakati Mtibwa wakiangusha alama mbili Jumapili iliyopita mbe...
Comments
Post a Comment