Mazishi ya mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Mwimbaji huyo aliyetesa kwa sauti yake tamu na kwa tungo zake za kusisimua, amezikwa katika makaburi ya Kisutu huku idadi kubwa ya wanamuziki wa fani mbalimbali ikiwa sehemu ya umati uliofurika makaburini hapo. Aidha, Dede pia amezikwa na vigogo wengi wa dini ya Kiislam, maofisa wengi wa serekali na wanamichezo maarufu. Pengine kwa miaka ya hivi karibuni, ukiondoka msiba wa marehemu Muhudini Gurumo, hakuna tena msiba wa mwanamuziki wa dansi uliohudhuriwa na watu wengi kama huu wa Dede. Mwili wa Dede ukiswaliwa swala ya mwisho katika msikiti wa Makonde, Kariakoo Safari ya kuelekea makauburini inaanza Umati wa watu ukiondoka Kariakoo kuelekea makaburi ya Kisutu Kila mtu alitamani kubeba...
Mwenyekiti wa zamani wa Simba Ismail Aden Rage ameipongeza Singida United kwa kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara ikiwa ni pamoja na kununua basi lao binafsi aliambia jana sarianews. Ilipofika kuhusu Singida United kucheza dhidi ya Simba, Rage amesema Singida hawataweza kuchomoka salama mbele ya mnyama. “Lazima tuwapongeze Singida United wameanza vizuri na watatupa ushindani, lakini wakikutana na timu yangu ya Simba wajue kipigo watakipata tu,” “Matayarisho yao yamenivutia hasa kitendo cha kutafuta basi zuri, hapo ndio kwenye uhaifu wa vialabu vingi ambavyo viongozi wetu wanakosa. Singida wanawathamini wachezaji wao, wangeweza kuzitumia hizo pesa kwa ujanja mwingine lakini wameamua kuwatafutia basi zuri la kisasa ambalo wachezaji watatumia.” Mkurugenzi wa Singida United Festus Sanga amesema, basi hilo limenunuliwa kwa shilingi milioni 350 za Tanzania na watalitumia katika safari zao za ndani na nje ya nchi. Sanga amesema fedhaimetoka ...
Arsene Wenger amemuorodhesha winga wa Manchester United Anthony Martial katika orodha yake ya washambuliaji anaotaka kuwanunua kiangazi hiki. Kocha huyo wa Arsenal ameanza kumkatia tamaa kinda wa Monaco Kylian Mbappe na sasa anampigia hesabu Martial. Wenger anajiandaa kulipa pauni milioni 40 kwa Martial, ambaye amekosa nafasi ya kudumu Old Trafford chini ya Jose Mourinho. Hata hivyo Wenger anahofia kuwa Mourinho anaweza kumbania kutokana na uhasimu mkubwa ulioko kati yake na kocha huyo wa Manchester United.
Comments
Post a Comment