Hatimaye jamii Forum kuto kutowa huduma inchini

Jukwaa maarufu nchini Tanzania Jamii Forums limekuwa miongoni mwa watoaji huduma za maudhui mtandaoni ambao wameathiriwa na kuanza kutekelezwa kwa sheria mpya za mtandaoni.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania imewataka watu ambao wamekuwa wakitoa imetoa ilani kwa wahudumu wote ambao bado hawajapata leseni kukoma kutoa huduma hizo kuanzia leo.
Mamlaka hiyo imesema wahudumu hao wana hadi Ijumaa wiki hii kuhakikisha wamejipatia leseni la sivyo watachukuliwa hatua.


TCRA imesema wanaoathirika ni wamiliki wote wa blogu, majukwaa ya mitandaoni, redio na televisheni.
Wameandika kwenye mtandao wao:
"Kutokana na notisi iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) leo Juni 10, 2018 inayotoa muda mfupi wa kututaka kusitisha utoaji huduma mara kabla ya Juni 11, 2018, tunalazimika kutii mamlaka na hivyo huduma hii haitapatikana kwa muda wakati tukifanya jitihada za kuhakikisha huduma inarejea.
"Kwa wateja wetu walio nchi nyingine, huduma hii itarejea mapema zaidi lakini kwa walio Tanzania kurejea kwa huduma kutategemeana na matokeo ya hatma ya jitihada za wawakilishi wetu walio Tanzania.
"Tunasikitika kuwa tunalazimika kufikia hatua hii ghafla lakini ni matumaini yetu kuwa wateja wetu mtaendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki."
Ujumbe wa mwisho kutoka kwa jukwaa hilo kwenye Twitter ulipakiwa usiku wa manane, na ulikuwa wa kutangaza taarifa hiyo kutoka kwa TCRA.
Mwanablogu Carol Ndosi ni miongoni mwa walioathiriwa na kuanza kutekelezwa kwa sheria hizo, mwanzoni aliomba ufafanuzi kuhusu wanaotakiwa kusitisha kuchapisha taarifa mtandaoni.
Baadaye, aliandika kwamba amelazimika kusitisha uandishi wa taarifa mtandaoni.
Taharifa na BBC

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger