Hatimae kocha wa Panone FC jumanne Ntambi amejiunga na mwadui fc kuchukua nafasi ya Ali Bushir






ALIYEKUWA kocha wa Panone FC, Jumanne Ntambi amejiunga na Mwadui FC kuchukua nafasi ya Ali Bushir aliyetupiwa virago. 


Ntambi aliyewahi kuifundisha Mwadui miaka ya nyuma, amesaini mkataba wa kukinoa kikosi hicho kwa msimu ujao. Katibu mkuu wa Mwadui, Ramadhani Kilao alisema Kocha huyo ataungana na Khalid Adam aliyekuwa kocha msaidizi wa Julio na Bushir. 





Alisema kuwa kati ya makocha hao, baada ya kusaini mkataba wanaangalia nani atakuwa kocha mkuu kwa sababu wote wanalingana kiwango cha elimu ambacho ni leseni ‘B’. “Baada ya kumuondoa Bushir tumemleta kocha mwingine anaitwa Ntambi, anaendelea na mazoezi na timu lakini kesho (juzi), ndio atasaini mkataba ila tutaangalia nani atakuwa kocha mkuu yeye na Khalid,” alisema Kilao.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger