Caf yasikia kilio cha Mourinho na Klopp

Kwa muda mrefu makocha wa ligi kubwa barani Ulaya wamekuwa wakulalamikia utaratibu wa chama cha soka Afrika CAf kufanya mashindano ya mataifa ya Afrika Afcon wakati ligi zikiwa zinaendelea.
Hii imekuwa ikizigharimu sana klabu za barani Ulaya kwa kuwakosa wachezaji wao muhimu wa Kiafrika wakati ligi ikiwa inaendelea lakini sasa shirikisho la mpira wa miguu Afrika Caf limesikia kilio cha vilabu hivyo.
Caf wameamua kuanzia sasa michuano hiyo mikubwa Afrika itakuwa ikifanyika mwezi June hadi July tofauti na mwanzo ambapo michuano hiyo ilikuwa ikifanyika kuanzia mwezi January hadi February.
Kuanzia mwaka 2019 ambapo mashindano hayo yatachezwa nchini Cameroon ratiba itabadilika huku timu zitakzoshiriki michuano hiyo nazo  zikiongezeka kutoka timu 16 kama ilivyokuwa mwanzo hadi timu 24.
Makocha wa vilabu vya Uingereza akiwemo Jose Mourinho na Jurgen Klopp walikuwa wahanga wakubwa wa michuano ya Afcon lakini sasa watakuwa wamesaidiwa kwa kiasi kikubwa kubaki na wachezaji wao.
Ratiba nyingine ikiwemo ile mashindano kufanyika kila baada ya miaka miwili imebaki paleplae huku wazo la kualika baadhi ya timu kutoka katika mabara mengine likifutwa na sasa timu zitakazoshiriki zinabaki vile vile kuwa za kutoka bara la Afrika.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger