Hatimae simba kusajili kiungo kipya kutoka Ghana taarifa zilizopo ni kwamba amepeleka kwa kambini afrika kusini



KLABU ya soka ya Simba ni kama imenogewa na wanandinga wa kutoka nchini Ghana ambapo sasa imeshusha straika mwingine na taarifa zilizopo ni kwamba amepelekwa kambini nchini afrika kusini.


Wachezaji wa wekundu hao kwa sasa wapo nchini Afrika Kusini kwa kambi ya siku 20 ya kujiandaa na Ligi Kuu sambamba na ile tamasha la kila mwaka la Simba Day linalofanyika kila ifikapo Agosti 8.


Taarifa za ndani zinazohusiana na masuala ya usajili zinasema kuwa raia huyo wa Ghana ni Thomas Agyei ambaye ni mpachika mabao ambaye Simba iliripotiwa kumtuma mjumbe mmoja kwenda kumalizana nae huko kwao.


 Agyei ambaye pia ni mchezaji kijana ameripotiwa kukamilisha hatua muhimu za kujiunga na kikosi cha Mnyama msimu huu ambapo mara baada ya kutaarifiwa ujio wake amekuwa akisubiliwa kwa hamu.



Habari ambazo bado ni motomoto zinasema kuwa kocha Joseph Omog ameridhishwa na kiwango chake kupitia CD ya aina ya uchezaji wake na ameuagiza uongozi ufanye hima kumpandisha pipa ili kuwahi kambi ya Sauzi.



Omog amehitaji uharaka wa kupelekwa kwa straika huyo kama njia ya kwenda kujiridhisha na kiwango katika kambi hiyo ya kujiandaa hatua ambayo uongozi umeitikia wito wa kocha wao huyo.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.