Vumbi kutoka mwenzini launzwa dola milioni 1.8 mjini New York

Mfuko moja uliotumika na mwananga Neil Amstrong kukusanya violezi vya mwezi umeuzwa kwa dola milioni 1.8 mjini New York.
Mfuko huo kutoka kwa chombo cha angani Apolo 11 mwaka 1969 ulinunuliwa katika eneo la Sotheyby na mtu asiyejulikana.
Mfuko huo bado una vumbi na mawe madogo madogo kutoka mwezini.
Mnada huo unajiri baada ya mapambano mahakamani kuhusu umiliki wa kifaa hicho cha kipekee kutoka kwa ujumbe wa Apollo 11 ambao ulikuwa katika mikono ya mtu binafsi.
Baada ya chombo hicho cha angani kurudi duniani, vifaa vyote vilipelekwa katika jumba la makumbusho la Smithsonian.
Hatahivyo mfuko huo uliwachwa katika boksi katika kituo cha vyombo vya angani cha Johnson kutokana na makosa ya kihesabu.
Baadaye haukutambulika wakati wa mnada wa serikali, ukiuzwa kwa dola 995 pekee kwa wakili mmoja wa Illinois 2015.
hatahivyo mamlaka inayosimamia vyombo vya angani Nasa ilijarabu kuuchukua mfuko huo, lakini mapema mwaka huu jaji mmoja aliamuru kwamba ulimilikiwa na mnunuzi huyo kimakosa ambaye baadaye ailiupeleka katika mnada huo wa Sutheby.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara