Done Deal: Yanga wamemtambulisha Ajib





Ibrahim Ajib ametambulishwa rasmi na klabu ya Yanga baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo kwenye mashindano mbalimbali kuanzia msimu wa 2017-2018.

Katibu Mkuu wa Yanga Charles Bonifasi Mkwasa na meneja wa timu Saleh Hafidh wamemtambulisha Ajib mbele ya waandishi wa habari ndani ya makao makuu ya Yanga mtaa wa Jangwani.






Awali zilianza kama tetesi huku Ajib na Yanga wote wakikanusha tetesi ambazo zilikua zikiibuliwa kwamba Ajib amesaini mkataba na Yanga.
Ajib amekabidhiwa jezi namba 10 ambayo ilikuwa inavaliwa na Matheo Anthony, Ajib ameondoka Simba akiwa anavaa jezi namba 23 ambapo kwa upande wa Yanga jezi hiyo inavaliwa na nahodha Nadir Harou ‘Cannavaro’.


Comments

Popular posts from this blog

Q Chillah ametambulisha wimbo mpya alioshirikishwa na rapa Chid Benz

Mbunge wa Nzega (CCM), Hussein Bashe ameshindwa kuvumilia

ATIMAE MOHAMED SALAH AVUNJA REKODI YA LIVERPOOL