KATIBU mkuu wa mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara, Yanga, Charles Boniface Mkwasa ametoa pole kwa wanachama wa klabu ya Simba kufuatia matatizo yaliyowakumba na kusababisha baadhi ya viongozi wake wa ngazi za juu kufikishwa kwenye vyombo vya dola.


 Baadhi ya viongozi wa juu wa klabu ya Simba ambao wapo mahabusu ni pamoja na rais wake, Evas Aveva na makamu mwenyekiti Geoffrey Nyange “Kaburu”.


 “Sisi wote ni familia ya soka hatuwezi kufurahia matatizo yanayowapata viongozi wa Simba wakati huu, suala hili limetugusa na tunawapa pole wanachama wao.”


 “Hatuna uadui nje ya uwanja, vita yetu ni ya kimpira tu, hivyo yanapotokea matatizo kama haya tunakuwa bega kwa bega katika kufarijiana na kutiana moyo,” alisema Mkwasa. Kesi ya viongozi hao imepangwa kusomwa tena Julai 20, mwaka huu kwenye mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger