Atimae taifa stars ya fuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano ya cosafa



Bao pekee la mshambuliaji wa Taifa Stars na klabu ya Dhofar ya Oman Elias Maguri limeiwezesha Stars kufuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano ya Cosafa.

Stars imepata ushindi wake wakati ikicheza dhidi ya wenyeji Afrika Kusini ambao ndio walikuwa mabingwa watetezi wa taji hilo.

Maguri amefunga bao hilo pekee dakika ya 18 kipindi cha kwanza baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa Mazamiru Yassin.

Baada ya mchezo, Maguri alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuonesha kiwango kizuri ikiwa ni pamoja na kufunga goli lililoisaidia Stars kufuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.

Stars itacheza na Zambia katika hatua ya nusu fainali baada ya Zambia wao kushinda 2-1 mchezo wao wa robo fainali walipo cheza dhidi ya Botswana.

Mechi ya nusu fainali ya Cosafa kati ya Taifa Stars dhidi ya Zambia itachezwa Julai 5, 2017.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.