MLINDA mlango mkongwe wa klabu ya Juventus Gianluigi Buffon amemshauri mlinzi wake katika timu ya taifa ya Italia Gianluigi Donnarumma kufuata matakwa ya moyo wake na kuachana na kelele anazopigiwa kwa sasa.





MLINDA mlango mkongwe wa klabu ya Juventus Gianluigi Buffon amemshauri mlinzi wake katika timu ya taifa ya Italia Gianluigi Donnarumma kufuata matakwa ya moyo wake na kuachana na kelele anazopigiwa kwa sasa.


 Buffon wenye umri wa miaka 39, aliibuka na ushauri huo kwa kinda Donnarumma mwenye umri wa miaka 18, aliyewaudhi mashabiki wa klabu anayoitumikia ya AC Milan baada ya kukataa kusaini mkataba mpya.



 “Donnarumma afuate kile ambacho moyo unataka,” alisema Buffon alipokuwa anahojiwa na Sky Sports. “Nilizungumza naye tukiwa na timu ya taifa kwa takriban robo saa na nikamweleza awe huru kuamua atakalo kwenye soka.


” Hata hivyo Buffon ameweka wazi kuwa hahitaji kuona kinda huyo akichukua ushahuri huo bila kufikiria kwa kina kwani huenda akazidisha hasira za mashabiki wa Milan ingawa angependa kumuona akitua Juventus na kuirithi nafasi yake

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.