Hatimaye Simba kukamilisha usajili wa kiungo wa yanga Haruna Niyonzima




Baada ya timu ya Simba kukamilisha usajili wa kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima usajili ambao ulikuwa unaogelewa sana na wapenzi wa Soka hapa nchi, taarifa mpya ni kwamba kiungo huyo atapewa jezi namba 8.

Kiungo huyo machachari ameacha na Yanga baada ya kucheza misimu sita mfululizo na amesajiliwa na Simba kwa mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya zaidi ya milioni 100 za Kitanzania.

Habari kutoka ndani ya Simba zinasema kuwa, Haruna atapewa jezi hiyo iliyokuwa ikitumiwa na Mwinyi Kazimoto.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kazimoto hayupo kwenye mipango ya mwalimu kwa msimu ujao baada ya mkataba wake kumalizika.

Haruna ambae ni kipenzi cha wana Yanga, atatumbulishwa rasmi na timu yake mpya katika sherehe za Simba Day Agosti, mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger