Marekani yaitungua ndege ya kijeshi ya Syria

Marekani imeitungua ndege ya kijeshi ya Syria iliyokuwa ikijiandaa kuwashambulia wanamgambo wa IS ambao wamekuwa wakihatarisha maisha ya wananchi wa nchi hiyo huku umoja wa mataifa ukitaka kuwepo na usuluhishi.

Aidha, Marekani imesema kuwa imefikia hatua hiyo mara baada ya jeshi la Syria kuvishambulia vikosi vya Syrian Democratic Force SDF, vinavyoungwa mkono na Marekani  kwa lengo la kupambana na wanamgambo wa Islamic State.

Kwa upande wa Serikali ya Syria imesema kuwa ndege yake ilikuwa katika maandalizi ya kuwashambulia wanamgambo wa Islamic State na si vikosi vya Syrian Democratic Force vinavyoungwa mkono na Marekani.

Vikosi vya Syrian Democratic Force (SDF ) vinaungwa mkono na umoja unaoongozwa na Marekani kwaajili ya kupambana na wanamgambo wa Islamic State ambao wamekuwa tishio katika ukanda huo.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger