Ramadhani Chombo aliyekuwa kiungo wa Mbeya City amesema hivi sasa yuko huru akisubiri timu inayoeleweka ili aweze kujiunga nayo





ALIYEKUWA kiungo wa Mbeya City, Ramadhani Chombo “Redondo” amesema kuwa hivi sasa yuko huru akisubiri timu inayoeleweka ili aweze kujiunga nayo msimu ujao.


 Kiungo huyo ambaye aliwahi kutiomkia Denmark wakati akiwa kwenye kituo cha Dyoc, amesema kuwa kuna timu zinamnyemelea lakini bado hawajafikia makubaliano. 


“Nipo huru hivi sasa, bado hakuna timu tuliyofikia makubaliano kwa ajili ya msimu ujao. Nasubiri kuona nini kitaendelea,” alisema Redondo.



 “Nipo kwenye mapumziko ya muda mfupi kabla ya kujua wapi nitaelekea msimu ujao, nitaweka wazi nikishafikai makubaliano na sehemu nitakayoenda,” alimaliza. Ramadhani Redondo aliwahi kuitumikia klabu ya Simba kabla ya kutimkia Mbeya City.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.