Man United yamsaini Victor Lindelof kwa pauni milioni 31

Manchester United wameafikia makubaliano ya kumsaini mlinzi raia wa Sweden Victor Lindelof kutoka Benfica kwa kima cha pauni milioni 31.
United wanasema kuwa kilichobakia ni makubaliano ya kibinafsi na uchunguzi wa kiafya ambavyo viitafanyika wiki ijayo.
Lindelof, ambaye ameichezea nchi yake mara 12 anatarajiwa kushiriki mechi ya kirafiki nchini Norway siku ya Jumanne
Mchezaji huyo mwenye maiak 22 ambaye amekuwa akiichezea Benfica tangu mwaka 2012 atakuwa mchezaji wa kwanza kusainiwa na Man U msimu huu.
Lindelof alicheza mara 47 klabu hiyo ya Ureno msimu uliopita.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.