Kauli za mawakili baada ya Malinzi na Mwesigwa kunyimwa dhamana


Baada ya mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kuwanyima dhamana Rais wa TFF Jamal Malinzi, Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa na afisa wa fedha Nsiande Mwanga, jopo la mawakili wa utetezi wameonekana kutoridhika na wateja wao kukosa dhamana.
“Washtakiwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani halafu wanaomba tena upelelezi wa kesi wakati suala tayari lipo mahakamani hiyo ndio pointi kubwa ambayo tumeiibua halafu kitu kingine tulichokiibua ni pamoja na maombi ya dhamana,”  Jarome Msemwa-wakili upande wa utetezi.
“Tumeiomba mahaka itoe dhamana kwa wateja wetu, kuna sheria ya Bunge inayokataza dhamana halafu kuna katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoruhusu dhamana. Kwa hiyo kwa amri ya mahakama ambayo imesomwa leo (jana) wateja wetu wanapelekwa rumande hadi Jumatatu Julai 3, 2017.”
“Sikutarajia katika muda na wakati kama huu kutakuwa na mashitaka yanayowakabili yanayofika 28 ya aina ileile lakini ndani yake yanatengenezwa machache kufanywa ya tutakatisha fedha wakati mashitaka yote tunayaona ni kughushi na kila kitu wanacho. Mimi sikutegemea kama watasema upelelezi haujakamilika wakati uchunguzi wao wamesema ni wa muda mrefu sana,” Aloyce Komba-wakili upande wa utetezi.
“Mvutano ulikuwa ni wa kisheria ambapo mwisho wa siku mahakama ikabidi ifanye maamuzi, sisi tulikuwa tunaomba dhamana vilevile kesi ianze kusikilizwa na tulikuwa tunasema hawawezi kusema upelelezi bado haujakamilika wakati wameshakamilisha kilakitu. Vilevile tukataka mtazamo huu ubadilike hapa nchini wa kuwaleta watu mahakamani halafu uchunguzi bado haujakamilika wanaishia kukaa ndani.”
Watuhumiwa wote walikana mashitaka yote 28 yanayowakabali hivyo kesi hiyo kuahirishwa hadi Jumatatu Julai 3, 2017

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.