Aliyekuwa gavana wa Rio de Janeiro afungwa miaka 14 kwa ufisadi

Aliyekuwa gavana wa jimbo la Rio de Janeiro nchini Brazil, amehukumiwa kifungo cha miaka 14 gerezani kwa ufisadi na ulanguzi wa pesa.
Sergio Cabral alihudumu mihula miwili kama gavana wa Rio kuanzia mwaka 2007 hadi 2014.
Analaumiwa kwa kupokea hongo kutoka kwa makampuni ya ujenza ili kuyapa zabuni za pesa nyingi.
Jaji Sergio Moro, alisema kuwa hakukuwa na ushahidi wa kutosha kumshtaki mkewe, Adriana Ancelmo
Cabral alikamatwa mwezi Novemba kama sehemu ya oparesheni iliyofahamka kama Car Wash, iliyohusu uchunguzi mkubwa, ambayo ilisababisha kukamatwa kwa wanasiasa mashuhuri na wafanyibiashara nchini Brazil.
Cabral ni mwanachama wa cham cha Democratic Movement Party, cha rais Michel Temer ambaye pia anafanyiw uchunguzi unaohusu ufisadi.
Jaji Moro alisema kuwa gavana huyo wa zamani alikuwa amechukua dola 813,000.
Hata hivyo jaji amesema kuwa pesa hizo hazijapatikana na huenda Cabral alizihamisha kabla ya akaunti zake kufungwa.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara