CHELSEA ‘MWENDOKASI’ KUWANASA ALEX SANDRO, TIEMOUÉ BAKAYOKO KUMPOZA ‘MBOGO’ CONTE!

MABINGWA WA ENGLAND Chelsea wanatarajiwa Wiki hii kuongeza kasi ya kuwanasa Alex Sandro wa Juventus na Tiemoué Bakayoko wa AS Monaco ili kumtuliza Meneja Antonio Conte ambae amepandwa na hasira kwa kutonunuliwa Mchezaji yeyote Mpya katika Walengwa wa Listi yake.
Conte, ambae yuko Vakesheni huko kwao Italy, alichukizwa na kutokuwepo na jitihada zozote na kukazuka habari ataondoka Chelsea kitu ambacho Klabu hiyo imekikana.
Inadaiwa Chelsea ilimtaka Conte auze baadhi ya Wachezaji waliokuwepo ilia pate Wapya na hilo likamsukuma kumtumia SMS Diego Costa kuwa hayumo kwenye mipango ya Chelsea na kumfanya Fowadi huyo alipue taarifa hiyo hadharani na kuibua msuguano mwingine kati ya Conte na Uongozi wa Chelsea.
Pengine hilo la kuondoka kwa Costa ndilo limewafanya Everton, wakijua wazi Chelsea wanamtaka Straika wao Romelu Lukaku, kudai Dau la Rekodi ya Dunia kumnunua Fowadi huyo wa Belgium alieazimwa toka Chelsea na kisha kuuzwa moja kwa moja kwa Bei chee.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.