Marekani yaitaka China kuikanya Korea Kaskazini

Marekani imeishinikiza China kuongeza jitihada zake katika kuizuia Korea Kaskazini kuendelea na mipango yake ya kinyuklia pamoja na utengezaji wa makombora.
Akizungumza baada ya kukutana na maafisa wakuu wa China, waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson amesema kuwa Beijing ina jukumu la kidiplomasia kuongeza shinikizo zaidi kwa Pyongyang iwapo ingetaka kupunguza wasiwasi katika eneo hilo.
Katika mkutano huo mjini Washington ambao ulihudhuriwa na waziri wa Ulinzi wa Marekani James Mattis bwana Tillerson alisema kuwa China inaunga mkono mpango wa Marekani wa kusitisha mpango wa kinyuklia wa Korea Kaskazini pamoja na majaribio ya makombora ya masafa marefu.
Pia ameyataka mataifa yote kuongeza juhudi za kumaliza biashara ya kihalifu ya Korea Kaskazini ambayo anasema inatumika kufadhili mipango yake ya Kinyuklia.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger