Kiwanya cha Garden Breeze cha Magomeni jijini Dar es salaam kitajazwa watu siku ya Idd Mosi





BENDI ya African Minofu imejinasibu kukijaza kiwanja cha Garden Breeze, Magomeni, Dar es Salaam kwa mashabiki wengi zaidi siku ya Idd Mosi pale watakapoporomosha burudani ya kukata na shoka. 


Bosi wa African Minofu, Matei Joseph aliiambia sarianews  kuwa, anaamini muziki watakaouporomosha utakuwa mkubwa kiasi cha kuchangia kukifanya kiwanja hicho kujaa mashabiki watakaovutwa na burudani yao. 


“Binafsi, ni msanii wa siku nyingi ninayefahamu mbinu nyingi za kimuziki, hasa katika kuwavuta mashabiki, hivyo naahidi kukijaza kiwanja hicho kwa muziki mnene zaidi,” amesema Matei.


 Matei amesema kuwa, shoo yao ya Idd Mosi katika kiwanja hicho imepangwa kuanza kurindima majira ya saa 12:30 jioni na kuendelea hadi majogoo, ambapo watatumbuiza vibao vyao vipya pamoja na vile vya zamani. 


Amesema kuwa pia watarindimisha nyimbo mbalimbali za kukopi kutoka mataifa mbalimbali, huku wakiahidi kuyapa kipaumbele maombi ya mashabiki pamoja na wapenzi wao watakaojitokeza kuhudhuria.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger