Atimaye Deus Kaseke anatarajia kuongeza mkataba wa miaka miwili kutumikia klabu ya Yanga




KIUNGO mshambuliaji wa klabu ya Yanga, Deus Kaseke anatarajia kuongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia timu hiyo iliyobeba ubingwa wa Ligi Kuu bara kwa mara tatu mfululizo.


 Kaseke aliyekuwa likizo kwao Mbeya, alirejea Dar es Salaam kuja kumalizana na uongozi wa Yanga baada ya kuwekewa mezani mkataba wa miaka miwili.


 “Hakuna sehemu yoyote nitakayosaini zaidi ya Yanga ambao nimemalizana nao katika kila kitu muhimu,” alisema kiungo huyo.


 “Yanga ni nyumbani, hizo taarifa za mimi kujiunga na Singida United nazisikia tu lakini ukweli ni kuwa ninasaini Yanga,” aliongeza. Dues Kaseke amekuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi cha George Lwandamina tangu alipotua akitokea timu ya Mbeya City.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara