uasi Bosco Ntaganda kutoa ushahidi

Aliyekua kiongozi wa waasi nchini Congo, Bosco Ntaganda anatarajiwa kutoa ushahidi leo katika mahakama ya kimatafa ya ICC.
Ntaganda aliyepewa jina la 'The Terminator ' atasimama kizimbani ikiwa ni takriban miaka miwili baada ya kesi kuanza.
Ntaganda anashutumiwa kutekeleza uhalifu na uhalifu dhidi ya binaadam unaodaiwa kutekelezwa na vikosi vyake.
Mashtaka yanasema kuwa kati ya mwaka 2002 na 2003 vikosi vyake vya uasi walivamia eneo la Ituri, wakatekeleza mauaji na vitendo vya kuwabaka raia.
Mwaka 2015, alikutwa na hatia kwa makosa 13 ya uhalifu wa kivita ikiwemo kuwasajili watoto wa umri wa chini ya miaka 15 kwenye jeshi na makosa mengine ya uhalifu dhidi ya binaadam.
Jopo lake la utetezi limepanga kuwaita mashuhuda 109 na wataalam wanne.Hii ndio sababu kesi hiyo inatarajiwa kuendelea kwa miezi kadhaa.
Ikiwa atakutwa na hatia atahukumiwa kifungo cha mpaka miaka 30 gerezani.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara