Marekani kuwawekea vikwazo washirika wa kibiashara wa Korea Kaskazini

Marekani inasema itaziwekea vikwaza nchi ambazo zinafanya biashara haramu na Korea Kaskazini, kwa mujibu wa waziri wa mashuri ya nchi za kigeni Rex Tillerson
Alisema kuwa Ikulu ya White House hivi karibuni itaamua ikiwa itaziwekea vikwazo nchi hizo.
Utawala wa Trump umeamua kuiwekea shinikizo zaidi Korea Kaskazini kufuatia na mpango wake wa nuklia.
Majaribio ya makombora ya hivi karibuni ya Korea Kaskazini ambayo yamepigwa marufuku naa Umoja wa Mataifa yamezua shutuma za kimataifa.


Korea Kaskazini inaaminiwa kupiga hatua katika kuunda makombora ya masafa marefu yenye uwezo wa kufika nchini Marekani.
Onyo la Bwana Tillerson lilitolewa wakati wa kikao cha bunge kuhusu mahusiano ya ya kigeni siku ya Jumanne.
Marekani haina uhusiano wa kibiashara na Korea Kaskazini na imekuwa ikitoa vitisho vya kuyawekea vikwazo mataifa ambayo yanafanya biashara na taifa hilo.
Hata hivyo Bwana Tillerso hakuzitaja moja kwa moja nchi hizo.
Alisema kuwa suala la Korea Kaskazini litazungumziwa na China, mshikika mkubwa wa Korea Kaskazini wakati wa mazungumzo wiki ijayo.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger