Timu ya Gor Mahia yatinga nusu fainali SportPesa

Gor Mahia imekuwa timu ya pili ya Kenya kutinga nusu fainali ya michuano ya SportPesa Super Cup.
AFC Leopards ndiyo timu ya kwanza ya Kenya kufuzu nusu fainali baada ya kuishinda Singida United na itacheza na Yanga hatua ya nusu fainali.
Gor Mahia imefuzu baada ya kuitwanga Jang'ombe Boys ya Zanzibar kwa mabao 2-0 katika mchezo wa robo fainali uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar.
Mnyarwanda mwenye asili ya Uganda, Meddie Kagere ndiye mfungaji wa mabao yote mawili katika dakika ya 66 na 78. Sasa Gor Mahia wanasubiri mshindi kati ya Simba dhidi ya Nakuru All Stars ya Kenya pia ambao umeanza tayari.

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

Atimae Singida United kuanza maandalizi yake kuelekea msimu mpya wa ligi kuu tanzania bara

Atimae Anthony Martian aongezwa katika orodha ya kusajiliwa katika msimu huu katika club ya Manchester United taharifa hiyo imetolewa na Arsene Wenger