Vodacom kuvunja rekodi ya mauzo ya DSE soko la awali

WAWEKEZAJI zaidi ya 40,000 wamevutiwa na hisa za Vodacom Tanzania PLC zinazoendelea na mchakato wa kuingia sokoni. Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao, alisema hisa hizo zitakuwa za kihistoria na zitavunja rekodi kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam kwa miaka 19 tangu kuanzishwa kwake.
Hii imechangia kwa kiasi kikubwa na malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kutaka kuona Watanzania wanakuwa wamiliki wa kampuni kubwa zinazofanya biashara nchini.
Biashara katika hisa za Vodacom Tanzania PLC kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam inatarajiwa kuanza mwezi huu baada ya kukamilika kwa taratibu za uhakiki unazofanywa na Mamlaka ya Masoko na Mitaji Tanzania (CMSA).
Katika taarifa yake, Ferrao alisema, “Vodacom Tanzania PLC inajivunia kuwa kampuni ya mawasiliano inayoongoza hapa Tanzania na ndiyo maana leo hii tumekuwa kampuni ya kwanza kutimiza masharti ya Bunge la Tanzania ya kutaka makampuni zote za simu za mkononi kuorodhesha hisa zake kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam.”
Vodacom Tanzania PLC kupitia kwa mshauri wake mkuu, kampuni ya Orbit Securities, imekabidhi kwa Mamlaka ya Masoko na Mitaji Tanzania (CMSA) majina ya wote walionunua hisa hizo kwa ajili ya,” alisema Ferrao

Comments

Popular posts from this blog

Siku ya jana yalifanyika maombi na mazishi mwimbaji mkongwe wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede aliyefariki Alhamisi asubuhi, yamefanyika leo saa saba mchana na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wakazi wa Dar es Salaam picha na sauti 5 bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe

MTIBWA Sugar FC iliangusha pointi za kwanza baada ya kucheza mchezo wa nne msimu huu. Baada ya kuzishinda timu tatu kutoka Kanda ya Ziwa (Stand United, Mwadui FC, Mbao FC) mabingwa hao mara mbili wa zamani walilazimika kusawazisha goli la Zubery Daby na kupata sare ya kufungana 1-1 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wao wa kwanza ugenini.